Habari za Simba
Habari za michezo

MANGUNGU ATOA KAULI YA KIBABE LEO SIMBA DHIDI YA POWER DYNAMO

Staff Desk September 16, 2023 12:53 pm

Mwenyekiti wa Simba SC, ametoa kauli ya kibabe kuelekea mchezo wao dhidi ya Power Dynamod majira ya saa 10 jioni hii leo Septemba 16, 2023.

“Simba ni timu kubwa kama inavyofahamika na watu wenye uelewa wa soka, hatuogopi kucheza na timu yoyote tumeshazifunga timu nyingi za Afrika Magharibi, Afrika ya Kaskazini na sasa tupo hapa Zambia kucheza na tutacheza na Power Dynamos ambao tulichezanao mechi ya kirafiki kwenye Simba Day.

Inaweza kuwa mechi ngumu kwa sababu tunacheza dhidi ya timu ambayo tumechezanayo katika kipindi kifupi kilichopita, watakuwa wamerekebisha makosa yaliyopelekea sisi tukashinda lakini naamini benchi letu la ufundi litakuja na mbinu za kuhakikisha tunashinda mechi hiyo,” alisema Mangungu

MASHABIKI WA YANGA KIGALI WAPATA ZALI HILI KUHUSU KUFELI KWA YANGA HERSI ASEMA MANENO HAYA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply