Home Azam FC HUKO LIGI KUU MAMBO NI MOTO, SIO SIMBA, YANGA WALA AZAM, MWAMBA...

HUKO LIGI KUU MAMBO NI MOTO, SIO SIMBA, YANGA WALA AZAM, MWAMBA HUYU HAPA

MAAFANDE WATEMBEZA KIPIGO...WANYEMELEA LIGI KUU...KITUO KINACHOFUATA PAMBA FC

Wenyeji, Mashujaa wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ihefu SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.

Mabao ya Mashujaa iliyopanda Ligi Kuu msimu huu yamefungwa na Omary Kindamba dakika ya 18 na Adam Adam dakika ya 80.

Kwa ushindi huo, Mashujaa wanafikisha pointi saba katika mchezo wa tatu na kupanda kileleni mwa Ligi Kuu wakizizidi pointi moja moja Yanga, Azam na Simba ambazo zimecheza mechi mbilimbili.

Kwa upande wao, Ihefu SC baada ya kipigo cha jana ambacho kinakuwa cha pili katika mechi tatu wanabaki na pointi zao tatu.

SOMA NA HII  GAMONDI AFANYA MAAMUZI MAGUMU MASTAA HAWA YANGA KUPINGWA PANGA.....UNAAMBIWA SKUDU NAE HANA BAHATI