Home Habari za michezo MANARA ARUKA NA SIMBA KISA INONGA

MANARA ARUKA NA SIMBA KISA INONGA

HAJI MANARA AUMBUKA...NI BAADA YA KUMGOMBANISHA RAISI YANGA NA MTANGAZAJI

Kutoka kwa El Bugatti Haji Manara baada ya kupost clip ya Mwenyekiti Wa Timu ya Simba Murtaza Mangungu akilalamika kuwa Inonga aliumizwa makusudi.

Ameandika Manara: “Inakuwaje Mcheza Rafu Mkuu wa Taifa akichezewa Rafu yeye iwe ni kusudi ila akicheza yeye iwe Damu ilikuwa imechemka?

“Beki gani anaemsogelea Inonga kwa kucheza mirafu ya kuumiza wengine katika Premier League ya Tanzania? Mmesahau alitaka kumvunja Sure Boy katika derby? Uliwasikia Viongozi wa Yanga wakisema ilikuwa kusudi au alitumwa?

“Tukemee Vitendo viovu uwanjani kwa team zote na Wachezaji wote bila kubalance Ukolo wa kimbumbumbu, eti kachezewa kusudi Rafu!

“Jana yake tu kabla ya hiyo Mechi, Mchezaji wa Mabingwa Lomalisa kachezewa Rafu kubwa kuliko hii, hatukusikia kina Hersi wakisema umbumbumbu kama huo,” ameandika Manara.

SOMA NA HII  BARCELONA KUMREJESHA MESSI...WAANDAA DONGE HILI NONO...HACHOMOI!!!