habari za simba
Habari za michezo

HAKUNA SILLAH WALA ONANA MWAMBA HUYU HAPA

Staff Desk October 16, 2023 11:02 am

Unaweza ukawa unajiuliza huyu Max Mpia Nzengeli hiki ambacho anakifanya Yanga ni kama vile mara yake ya kwanza ila hapana; huyu mwamba huu ni mwendelezo wake.

Maana msimu uliopita kabla ya Ligi Kuu ya nchini DR Congo (Linafoot) haijasimama Mbappe wa Bongo Max Nzengeli katika mechi 8 alifunga magoli 4 na kutoa Assist tatu ambapo jumla alihusika katika magoli 7.

Msimu huu wa kwanza akiwa na Mabingwa watetezi Yanga anafanya mwendelezo wa kile ambacho ametoka nacho kule DR Congo,Hadi sasa Max Mpia Nzengeli amehusika katika mabao matano kwenye mechi 5. Jamaa amefunga goli 3 na Assist 2,What a Player!!

Hiki anachokifanya Mbapee wa Bongo sifa kubwa ziende kwa Rais wa Yanga Eng Hersi Said na watendaji wake ambao walifanya saka nyoka na kwenda kusajili hiki kipaji kutoka DR Congo. Hadi sasa Max Nzengeli ndio usajili bora nchini hakuna Willy Onana wala Gibril Sillah.

KUMEKUCHA…….MANULA APEWA RASMI AL AHLY KUMEKUCHA FEI TOTO ATAKA KULIANZISHA TENA AZAM, ADAI HANA FURAHA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply