Home Habari za michezo MWANA FA AWEKA WAZI WALICHOCHANGIA SIMBA

MWANA FA AWEKA WAZI WALICHOCHANGIA SIMBA

WAZIRI

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma maarufu kama Mwana FA amesema kuwa iwapo kuna timu inataka kutoa chochote kwa ajili ya kusaidia maboresho ya uwanja wa Mkapa, basi inakaribishwa.

Mwana FA amesema hayo leo wakati akizungumza kwenye kipindi cha Kipenga Extra, East Africa Radio.

“Katika ukarabati wa uwanja wa Mkapa Simba wamechangia kwa kuweka TV mpya pamoja na Fridge mpya.

“Hivyo kwa wanaoona kwamba Simba Sports Club hawatakiwi kuvimba (Wanafaidi) basi na wao watafute kitu cha kuleta ili wote wawe sawa kwani milango ipo wazi,” amesema Mwana FA.

SOMA NA HII  DILI LA MAYELE KUTUA AFRIKA KUSIN LAMFIKIA 'PROFESA' NABI...NA HAYA NDIO MAJIBU YAKE....