Habari za Yanga
Habari za michezo

MOMO AWASHAURI VIONGOZI WA SIMBA, HERSI WA YANGA ATAJWA

Staff Desk November 11, 2023 10:39 am

Mchambuzi kutoka Wasafi Fm Ricardo Momo amewapa ushauri viongozi wa Simba wajifunze kwa Rais wa klabu ya Yanga SC Injinia Hersi Said namna ambavyo anaendesha timu.

Ricardo amesema Hersi ndani ya muda mfupi ameweza kutengeneza historia ndani ya Klabu ya Yanga kwa kufanya mambo mengi muhimu kwa ajili ya Wapenzi na wanachama wao.

Mchambuzi huyo amegusia usajili Bora ambao Hersi uwewawezesha kufika fainali ya kombe la Shirikisho na kufuzu hatua ya makundi ligi ya Mabingwa baada ya miaka 25.

Aidha, Momo amesema Yanga wameweza kumfunga Tano mtani ni jambo kubwa na la kihistoria kwa vilabu hivyo.

“Yanga pia wameweza kuchaguliwa kuwania timu Bora ya mwaka katika tuzo za CAF hiyo inaletwa na Uongozi bora.”

Momo amewashauri na Viongozi wa Simba kUbadili mfumo wao wa kuendesha klabu hili kupata mafanikio zaidi.

UBABE WA YANGA UPO KWENYE UTATU HUU WA MAP YANGA BADO ANAMSAKA PACHA WA MAYELE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply