Home Habari za michezo HUKO YANGA UNAAMBIWA UBABE UBABE TU

HUKO YANGA UNAAMBIWA UBABE UBABE TU

Habari za Yanga

Vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara Timu ya Yanga imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC kwa kufikisha alama 24 baada ya michezo 9.

hiyo ni baada ya kuichapa Coastal Union bao 1-0 katika mchezo mgumu uliopigwa Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.

Bao pekee la ushindi la Yanga katika mchezo wa leo limefungwa na Clement Mzize alieingia kutokea benchi akichukua nafasi ya Kennedy Musonda.

Bado mambo yanazidi kuwa magumu kwa Coastal Union ambao katika michezo yao 9 wamshinda mchezo mmoja pekee.

SOMA NA HII  MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA ALHAMISI