Home Habari za michezo BENCHIKHA:- HAWA APR HAWA NI BALAAHA NA NUSU….

BENCHIKHA:- HAWA APR HAWA NI BALAAHA NA NUSU….

Habari za Simba leo

Kocha Mkuu wa Simba, Abdelhak Benchikha amesema APR ni timu bora na imempa kipimo kizuri cha kujua uimara wa kikosi cheke ulivyo kwa sasa.

Benchikha amesema APR wanacheza vizuri kuanzia kwenye kuzuia mpaka kushambulia wapo vizuri kwenye kuziba mianya wakati wanaposhambuliwa.

Akizungumzia mchezo wenyewe Benchikha ameongeza kuwa ulikuwa mzuri na Simba ilijitahidi kufanya kila tuliloweza kupata goli lakini wamekutana  na timu bora.

“APR ni timu nzuri, inacheza soka safi. Ipo vizuri kwenye kuzuia pamoja na kushambulia lakini nasi tulikuwa vizuri ndio maana hakuna aliyefungwa.”

“Matokeo ya sare yalistahili kila timu ilikuwa bora, tunaenda kujipanga kwa ajili ya mchezo wa robo fainali,” amesema Benchikha.

SOMA NA HII  BAADA YA KUFUZU MAKUNDI CAF...BEKI YANGA 'ALAMBA MCHANGA' KULETA MAKUBWA ZAIDI...