Home Habari za michezo KUHUSU ENG HERSI KUVAMIA MAJUKUMU YA CEO….UKWELI USIOSEMA HUU HAPA…SENZO ALIMKIMBIA..

KUHUSU ENG HERSI KUVAMIA MAJUKUMU YA CEO….UKWELI USIOSEMA HUU HAPA…SENZO ALIMKIMBIA..

WAKATI Leseni za klabu zikianisha juu ya timu kuajiri mtendaji mkuu wa ajili ya kufanya kazi za mbalimbali lakini kwa Yanga ni tofauti baada ya mtendaji wao Andre Mtine, raia wa Zambia ni tofauti na mtangulizi wake aliyepita ndani ya klabu hiyo Senzo Mbatha.

Taarifa za uhakika kuwa majukumu yote ndani ya klabu hiyo anafanya Rais wa klabu hiyo, Hersi Said ikiwemo suala la usajili, mambo ya utendaji na ndiyo chanzo cha Senzo kuondoka, maana alijiona ni CEO kivuli.

Mtoa habari huyo amesema kulingana na hali hiyo ambayo ilimshinda Senzo anakuja kukutana nayo Mtine ameonekana kuridhia na hali hiyo ya kuwa mtendaji kivuli.

“Ni kweli Mtine amekubali kuridhika na jinsi ambavyo Yanga inavyoendesha na kufanya majukumu machache huku mengi ambayo anatakiwa kufanya, majukumu hayo hufanya Rais,” amesema Mtoa habari huyo.

Mtoa habari huyo amesema mara kadhaa katika mambo mengi yanayomuhusu  CEO huoneka kufanya Rais wa timu kuliko mwenye majukumu yake tofauti na ilivyo kwa watendaji wa klabu zingine kama ilivyo kwa Simba, Iman Kajula akitimiza majukumu yake.

Amesema imekuwa tofauti na CEO wa timu zingine ikiwemo wapinzani wao Simba amekuwa akifanya majukumu yake kwa kuonekana mara kadhaa katika utendaji wake kazi kuliko Yanga.

Mtine ambaye amekuwa akionekana mara nyingi uwanjani hasa timu yao inapocheza lakini mara chache kuonekana katika majukumu yake

SOMA NA HII  EDO KUMWEMBE:- SIMBA INAWEZA ISIPITE ....KIBU DENIS SIO MIQUISSONE...HAWANA IMANI NA BOCCO...

2 COMMENTS