Kwenye mchezo dhidi ya Jamhuri ,Yanga walicheza kawaida ila walikutana na timu ya kawaida wakaifunga magoli matano,mchezo dhidi ya Jamus walipata shida kupata ushindi na ushindi ulikuja dakika za lala salama
Jana dhidi ya APR ilikuwa moja kati ya mechi nzuri na wamefungwa magoli matatu .
Kipindi cha kwanza Yanga walitawala na waliona game kama rahisi ,back pass zilikuwa nyingi hata sehemu ambazo hazikuwa na ulazima
Goli la kusawazisha la APR ndio liliwarudhisha mchezoni na kama wangekuwa na utulivu zaidi ule mnara wa 5G ungesimama jana
Msheri alikuwa nje muda mrefu hajacheza lakini kiwango alichoonesha anaonekana kabisa huyu ana kitu,Naanguka pia alikuwa na game nzuri sana na mwingine ni Shekhani hata alivyoingia aliongeza kitu
Wachezaji hawa wamepewa nafasi na wameonesha wanakitu,Yanga itaangalia inawatumiaje
Lakini kuna wachezaji wazoefu kama Ngushi ,Mauya na Mkude wameiangusha Yanga kwa kweli
Ukiacha magoli mawili aliyofunga mechi ya kwanza ,mechi zingine ameonesha kwanini anakaa nje na Mashabiki wamepata majibu kwanini hawa wanakaa nje