Home Habari za michezo BAADA YA KUKIWASHA KWENYE CAF ….YANGA WABARIKI PACOME, MAXI KUPIGWA BEI…

BAADA YA KUKIWASHA KWENYE CAF ….YANGA WABARIKI PACOME, MAXI KUPIGWA BEI…

Habari za Yanga SC

Yanga SC wameeleza kuwa wapo tayari kumuuza Max Nzengeli pamoja na wachezaji wengine wowote wanaofanya vizuri endapo itatokea timu inawahitaji.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ali Kamwe ametoa kauli hiyo alipokuwa Afrika Kusini walipokwenda kuwavaa Mamelodi Sundowns katika mchezo wa pili ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kutoka sare ya bila kufungana katika mchezo wa awali uliopigwa Benjamini Mkapa Stadium.

“Sisi hatuna hofu ya wachezaji wanaofanya vizuri kuondoka, tulimuuza Fiston Mayele akiwa mfungaji bora hivyo sisi hatuna shida. Wakitokea watu wanawahitaji wataweka mpunga tutaleta wachezaji wengine na maisha yataendelea kama kawaida,” alisema Kamwe.

SOMA NA HII  WANAJESHI WA MPAKANI, KAZINI LEO KIMATAIFA