Home Habari za Yanga Leo SERIKALI YAINGILIA KATI MGOGORO SIMBA…DKT NDUMBARO ATOA KAULI

SERIKALI YAINGILIA KATI MGOGORO SIMBA…DKT NDUMBARO ATOA KAULI

Habari za Simba Leo

WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro, ameipongeza Yanga kwa mafanikio makubwa, chini ya Rais wa klabu hiyo, injinia Hersi Said, akiwataka Simba Kuondoa migogoro iliyopo ndani ya klabu yao ili kufikia mafanikio ya malengo yao.

Dkt Ndumbaro ambaye pia ni mwanachama wa Simba SC, alisema kwamba Yanga na Azam FC zimeongeza ubora wao, ila  Simba hajashuka kiwano, lakini anashangaa ni kwanini kumekuwa na migogoro katika klabu hiyo.

“Siamini kama Simba ni mbaya, isingefika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, shida ninayoiona ni ubora wa Yanga na Azam, hivyo ijifunze na ikajipange upya, shida ya Simba na Yanga mojawapo ikiwa vizuri nyingine inaibua migogoro, hivyo zinatakiwa kubadilika,”

Hata Hivyo Dkt Ndumbaro aliwataka Wanachama na Mashabiki wa Yanga wajitahidi kumlinda Injinia Hersi kwa mafanikio wa klabu yao na maendeleo ya mpira wa miguu nchini.

 

“Mafanikio hayamei kama udongo, isipokuwa yamejengwa na kuleta na watu, hivyo nimpongeze injinia na mdhamini wao GSM,Yanga imekuwa bora ndio maana iliweza kufika fainaliza Kombe la Shirikisho Afrika na isingenyimwa bao dhidi ya Mamelodi ingecheza fainali za Ligi ya Mabingwa Afrika,”

Pia hakusita kuisifia fainali ya Kombe la Shirikisho (FA) iliyochezwa Yanga dhidi ya Azam kwamba dakika 120, watu walikuwa hawatulii kwenye viti.

“Nilikuwepo uwanjani, nilikaa na injinia, muda wote alikuwa anapiga kelele, nikamwambia tulia dawa ikuingie, lakini yote kwa yote nampongeza kwa kuchukua ubingwa huo,” amesema

SOMA NA HII  YANGA YAPELEKA MWINGINE AZAM...MWENYEWE AFUNGUKA