Home Uncategorized DUH HAWA NDIO WABAYA WA YANGA LEO UWANJA WA TAIFA

DUH HAWA NDIO WABAYA WA YANGA LEO UWANJA WA TAIFA


 1959 ni mwaka ambao Township Rollers ilianzishwa nchini Botswana na leo itamenyana na Yanga uwanja wa Taifa majira ya saa 12:00


Jumla ya mataji 15 imetwaa na inatumia mfumi wa 4-3-3 na inapenda kushambulia kwa kutumia njia ya pembeni.

Washambuliaji wao wakali ni pamoja na Ditlhokwe, Joel Morogosi wanapenda kukaa mbele peke yao wakisubiri mashambulizi ya kushtukiza.
 

Leo wanamnyana na Yanga, ambao mwaka 2018 kwenye michuano ya kimataifa iliwatoa Yanga kwa kuwafunga mabao 2-1 uwanja wa Taifa kabla ya kulazimisha sare tasa Botswana.

Wametia Bongo Juzi wakiwa wamebeba maji yao pamoja na Juice ili kukwepa hujuma za mwanzo tayari wameshawasoma wapinzani wao kupitia video mbalimbali,

Ikumbukwe pia ilicheza mchezo wa kirafiki na watani wa Yanga, Simba, nchini Afrika Kusini na ililazimisha sare ya kufungana bao 1-1.

SOMA NA HII  SABABU KUU TATU ZILIZOPELEKEA SIMBA KUFUNGWA NA UD SONGO - VIDEO