Simba SC

Mbili Za Ligi Kuu Zamuwania Ladaki Chasambi

Vardo July 11, 2026 11:12 am

KIUNGO wa Simba, Ladaki Chasambi huenda akaitumikia Mashujaa au Pamba Jiji kwa mkopo msimu ujao ikiwa ni sehemu ya mpango wa kumpa nafasi ya kucheza mara kwa mara baada ya kushindwa kupata namba kikosini hapo.

Chasambi alijiunga na Simba Januari 8, 2024 akitokea Mtibwa Sugar kwa mkataba wa miaka mitatu unaotarajiwa kumalizika Desemba 2026, hivyo usajili ujao wa dirisha dogo atakuwa huru.

Taarifa zinaeleza uongozi wa mchezaji huyo ulianza kutazama uwezekano wa kumrejesha Mtibwa Sugar, lakini baada ya klabu hiyo kushuka daraja, sasa unaelekeza nguvu Mashujaa au Pamba Jiji ambazo zimeonyesha utayari wa kumpokea.

Chasambi amekuwa akipata ushindani mkubwa wa nafasi ndani ya Simba, hasa baada ya ujio wa kocha Steve Barker, ambapo analazimika kuwania namba na viungo Libase Gueye, Elie Mpanzu na Inno Loemba ambao wamekuwa wakionyesha kiwango kizuri na kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara.

Msimu uliopita chini ya kocha Fadlu Davids, kiungo huyo alikuwa akitumika katika nafasi mbalimbali, ikiwemo kubadilishwa na kucheza beki wa kulia.
Hata hivyo, ujio wa kocha mpya na kuongezeka kwa ushindani ndani ya kikosi cha Simba kimemfanya mchezaji huyo kutafuta njia mbadala ya kurejea kwenye kiwango chake ambapo ni kutoka kwa mkopo.

“Tunatamani acheze na arudi kwenye kiwango chake, kukaa benchi muda mrefu kumemrudisha nyuma hivyo tumeona ni sahihi yeye kwenda kwa mkopo acheze angalau,” kilisema chanzo hicho na kuongeza.

“Mtibwa tulitaka kumrudisha lakini matamanio yetu pia acheze Ligi Kuu ili aonekane na kurudi kwenye kiwango chake. Kama tutapata nafasi Mashujaa atarejea, kama itashindikana tutaangalia namna nyingine.”
Kalesto Afungua Njia Ya Loemba Kuondoka Simba. ‘Play Off’ Polisi TZ Katika Njia Za Ihefu Na Mashujaa? Prisons Ni Heshima Tu