O’reilly: Nafurahi Kumkabili Messi
ATLANTA, MAREKANI: BEKI wa kushoto wa England, Nico O’Reilly, amesema anaiona mechi ya nusu fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Argentina kama fursa ya kipekee ya kumkabili Lionel Messi, ambaye anaamini ni mchezaji bora zaidi kuwahi kucheza soka.
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Messi kucheza dhidi ya England, na akiwa na umri wa miaka 39, huenda ikawa pia mara yake ya mwisho kukutana na timu hiyo. O’Reilly, ambaye pia ni beki wa Manchester City, hajawahi kukutana na Messi katika ngazi ya klabu.
Akizungumza na BBC Radio 5 Live, O’Reilly amesema:
Messi alianza mashindano haya kwa kufunga mabao matatu (hat-trick) katika ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Algeria. Katika mechi hiyo aliweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote katika historia ya Kombe la Dunia, akiifikia rekodi ya mabao 16 iliyokuwa ikishikiliwa na Miroslav Klose tangu mwaka 2014.
Kwa upande wake, kipa wa England Jordan Pickford amesema licha ya ubora wa Messi, timu yake haiwezi kuelekeza nguvu zote katika kumzuia yeye pekee.
“Messi amefunga mabao mengi sana na amechangia mafanikio mengi katika maisha yake ya soka. Ni jambo zuri hatimaye kupata nafasi ya kucheza dhidi yake baada ya kumtazama tangu nilipokuwa mtoto,” amesema Pickford.
“Sote tunajua Messi ni mchezaji wa kiwango cha juu, lakini pia tunajua Argentina ina wachezaji wengi wazuri. Hatuwezi kujikita tu katika kumzuia Messi. Tunapaswa kuzingatia pia nguvu zao nyingine na kutumia udhaifu wao kwa manufaa yetu.”
Mshindi wa mchezo huo wa nusu fainali atakutana na mshindi kati ya Ufaransa na Hispania, ambao walicheza nusu fainali nyingine jana, katika fainali ya Kombe la Dunia itakayofanyika Jumapili, Julai 19, 2026 kwenye Uwanja wa New Jersey.