Nyota huyo ameaminiwa na kocha, Juma Mgunda, licha ya uwepo wa washambuliaji wengine wakiongozwa na mkongomani mwenzake, Heritier Makambo aliyetoka TRA United zamani Tabora United na Abdulaziz Shahame ‘Haaland’, aliyetokea kikosi cha TMA FC.
Ngoy alijiunga na Namungo msimu wa 2023-2024, akitoka Kitayosce iliyobadilishwa jina na kuitwa Tabora United na sasa TRA United, baada ya kuifungia mabao 15 ikiwa Ligi ya Championship, nyuma ya kinara, Edward Songo wa JKT Tanzania aliyefunga 18.
Mshambuliaji huyo alitua hapa nchini kwa mara ya kwanza msimu wa 2022-2023, akitokea Real Nakonde FC ya Zambia na msimu wa 2023-2024, alifunga bao moja tu, huku 2024-2025, akifunga mawili na sasa msimu wa 2025-2026, tayari amefunga manane.