Friday, March 6, 2026
Home Blog

TENGENEZA PESA NA EARLY PAYOUT LEO

0

Je unajua kuwa leo hii unaweza kutengeneza pesa na Meridianbet haraka sana kupitia chaguo la EARLY PAYOUT. Chagua mechi zako sasa na ubashiri ndani ya Meridianbet.

Meridianbet, inaendelea kutoa huduma mpya ya Early Payout, inayolenga kuboresha uzoefu wa wateja wake na kuhakikisha ushindi unapatikana haraka zaidi. Huduma hii ni suluhisho la kipekee kwa wapenzi wa kubashiri, kwani inawawezesha kulipwa mapema kabla ya mchezo kumalizika, mradi timu wanayobashiri ipo kwenye nafasi nzuri ya kushinda.

Wateja wanaweza kufurahia ushindi wao ikiwa timu zao zinashika nafasi nzuri, bila kusubiri dakika 90 kumalizika au matokeo rasmi. Hii ni fursa ya kipekee kwa wateja wa Meridianbet kuendesha mikakati yao ya kubashiri kwa ujasiri zaidi na kudhibiti hatari.

Chaguo hili linapatikana kwenye mechi za mpira wa miguu pekee ambapo mchezaji ili ashinde kwa Early Payout inabidi abashiri timu moja iongoze kwa magoli mawili na ushindi unahesabika kabla hata ya mechi kumalizika.

Pia Meridianbet inasema kuwa huduma hii inatumika kwenye ligi zote muhimu ndani na nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na Premier League, La Liga, Serie A, Bundesliga na mashindano makubwa ya kimataifa. Meridianbet inatambua umuhimu wa wateja wake, na Early Payout ni njia ya kuhakikisha unapata furaha na ushindi haraka zaidi.

Ukiachana na promosheni hiyo, Meridianbet inakwambia tengeneza mkwanja kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mteja wa Meridianbet anakumbushwa kuwa mechi za (Live) ambazo zinaendelea huruhusiwi kubashiri kwa kutumia Early Payout lakini CASHOUT inapatikana hivyo mteja anaweza akatoa pesa yake sasa akibashiri kwa kutumia chaguo hilo hapo.

Meridianbet inahimiza wateja wote kujiunga sasa, kujiandikisha na kuweka dau kwenye mechi yoyote inayopatikana kwenye jukwaa la Meridianbet. Kwa wateja wapya na wateja wa zamani, hii ni fursa ya kipekee ya kujaribu ushindi wa haraka na kuendelea kufurahia bonasi na promosheni mbalimbali zinazotolewa na kampuni.

Kwa kuwa Meridianbet inajivunia kutoa odds bora na teknolojia za kisasa, huduma ya Early Payout ni hatua nyingine ya kuimarisha uhusiano wa kampuni na wateja wake Tanzania. Kampuni inaendelea kuwekeza kwenye ubunifu na ubora, kuhakikisha kila mbashiri anapata uzoefu wa kipekee, usalama wa malipo, na msisimko wa ushindi haraka zaidi.

Unangoja nini sasa, bashiri na Early Payout ndani ya Meridianbet ujiweke kwenye nafasi ya kushinda pesa leo.

NSAJIGWA AANZA POINTI MOJA PRISONS, IBENGE AKUNJA SURA

0

Wakati Azam FC ikinung’unika na sare ya pili mfululizo, Tanzania Prisons ni kicheko kwa kupata pointi moja dhidi ya wapinzani wao hao katika mechi ya Ligi Kuu Bara.

Kabla ya mechi hiyo iliyopigwa leo Machi 5, 2026 kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Azam ilitoka kupata pointi moja kwenye sare ya 2-2 dhidi ya Pamba Jiji huku Prisons ikilala 2-0 kwa Simba.

Mechi hiyo ilikuwa wa kwanza kwa Kocha Shadrack Nsajigwa tangu kutambulishwa Tanzania Prisons akichukua mikoba ya mtangulizi wake, Zedekiah Otieno raia wa Kenya.

Kipindi cha kwanza timu zote zilicheza kwa tahadhari na mashambulizi ya kushtukiza lakini ilishuhudiwa dakika 45 za kwanza zikiisha kwa nguvu sawa bila kufungana.

Hata hivyo, Azam itajilaumu zaidi kufuatia nafasi za mipira ya kutenga kutoitumia vyema baada ya mashuti yote kutokuwa na madhara langoni mwa Prisons.

Kipindi cha pili, Azam ilionekana kutawala mechi kwa mashambulizi ya mara kwa mara, huku Prisons ikifanya jukumu la kuokoa zaidi hatari haswa kipa wake Mussa Mbisa aliyesimama imara golini.

Dakika ya 77, Prisons iliamua kufanya mabadiliko ya kiufundi kwa kumpumzisha Lambart Sabiyanka aliyempisha Samson Mbangula na Never Kagoma akichukua nafasi ya George Mpole.

Mabadiliko hayo yaliipa nguvu Maafande hao haswa eneo la ushambuliaji ambapo Mbangula aliweza kuwapa ugumu mabeki kwa kosa kosa dhidi ya kipa Aish Manula ikiwamo dakika 90 walipomkosa kipa huyo kwa kuokoa shuti la Never.

Azam pia ilifanya mabadiliko kwa kumtoa Zidane Sereri na nafasi yake kujazwa na Albogast Kyobya huku James Akaminko akimpisha Sadio Kanoute, lakini ubao ukabaki vilevile.

Kocha Mkuu wa Azam, Florent Ibenge, amesema sare hiyo si matokeo mazuri kwao baada ya kupata matokeo kama hayo dhidi ya Pamba Jiji akieleza kuwa bado hawajakata tamaa kwakuwa Ligi haijaisha.

Amesema walikuwa na matarajio ya ushindi kutokana na maandalizi lakini nyota wake walipambana wakakosa umakini wa kutumia nafasi za mabao walizopata.

“Si matokeo mazuri kwetu kwakuwa tuliumudu mchezo lakini licha ya jitihada za wachezaji ila hawakuweza kutumia vyema nafasi walizopata kufunga mabao, nitalifanyia kazi kwa mechi zijazo,” amesema Ibenge.

Kocha Mkuu wa Prisons, Shedrack Nsajigwa, amesema pointi moja kwao si mbaya hapo kuwa walihitaji ushindi akikiri kuwa bado wanao wakati mgumu kupambana kila mechi.

“Uwanja pia haukuwa mzuri lakini nishukuru kwa matokeo haya kutokana na ugumu wa Azam na ubora wao, tunaenda kujipanga kwa mechi zijazo,” amesema Nsajigwa.

MKONGOMANI NAMUNGO AWEKEWA MKATABA MPYA

0

UONGOZI wa Namungo FC, uko katika mazungumzo ya kumwongezea mkataba mpya mshambuliaji wa kikosi hicho, Mkongomani, Fabrice Ngoy, baada ya mabosi wa timu hiyo kuridhishwa na kiwango chake.

Akizungumza na Soka la Bongo, Mratibu wa Namungo, Ally Suleiman alisema mazungumzo na nyota huyo ili kuongeza mkataba mpya yameanza na yamefikia katika hatua nzuri, baada ya kuridhishwa na kiwango chake tangu amejiunga na kikosi hicho.

“Tumeanza taratibu mapema ili kuepusha migongano inayoweza kutokea mwishoni mwa msimu baada ya mkataba wake kuisha, ni mchezaji mzuri ambaye tunaamini kwa kipaji na umri wake atatusaidia sana katika michuano mbalimbali,” alisema Suleiman.

Kwa upande wa mshambuliaji huyo ambaye kwa sasa ndiye anayeongoza chati ya ufungaji katika Ligi Kuu Bara msimu huu kwa kufunga mabao mengi akiwa nayo manane, alisema suala la hatima yake ni mapema kulizungumzia, japo malengo yake ni kuendelea kufanya vizuri.

Nyota huyo ameaminiwa na kocha, Juma Mgunda, licha ya uwepo wa washambuliaji wengine wakiongozwa na mkongomani mwenzake, Heritier Makambo aliyetoka TRA United zamani Tabora United na Abdulaziz Shahame ‘Haaland’, aliyetokea kikosi cha TMA FC.

Ngoy alijiunga na Namungo msimu wa 2023-2024, akitoka Kitayosce iliyobadilishwa jina na kuitwa Tabora United na sasa TRA United, baada ya kuifungia mabao 15 ikiwa Ligi ya Championship, nyuma ya kinara, Edward Songo wa JKT Tanzania aliyefunga 18.

Mshambuliaji huyo alitua hapa nchini kwa mara ya kwanza msimu wa 2022-2023, akitokea Real Nakonde FC ya Zambia na msimu wa 2023-2024, alifunga bao moja tu, huku 2024-2025, akifunga mawili na sasa msimu wa 2025-2026, tayari amefunga manane.

DODOMA JIJI, JKT TZ KUANZA MSAKO WA CAF

0

TIKETI ya kuisaka michuano ya kimataifa msimu ujao, inaanza leo Ijumaa kwa mechi za raundi ya 32 bora ya Kombe la Shirikisho la CRDB, huku JKT Tanzania, Dodoma Jiji na TRA United zinazoshiriki Ligi Kuu Bara, zikishuka viwanja mbalimbali.

JKT Tanzania iliyoichapa Pan African mabao 7-0, katika mechi ya raundi ya 64 bora, itakuwa kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam kucheza dhidi ya Hausung FC ya Njombe, iliyoitoa West Singers ya jijini Mwanza kwa kuichapa mabao 2-1.

Kwenye Uwanja wa Black Rhino jijini Arusha, wenyeji TRA United iliyoitoa Rhino Rangers ya Tabora kwa bao 1-0, itacheza dhidi ya Kijiwe Nongwa ya Songwe, iliyoichapa Barberian FC kwa penalti 4-2 baada ya sare ya 1-1 ndani ya dakika 90.

Mechi ya mwisho leo itapigwa Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma na Dodoma Jiji baada ya kuitoa Kilimanjaro Wonders ya Kilimanjaro kwa kuichapa mabao 3-1, inakutana na African Sports ya Tanga iliyoitoa Kilimo FC ya Singida kwa mabao 4-1.

Kocha wa Dodoma Jiji, Amani Josiah alisema licha ya heshima kubwa kutokana na bingwa kupata nafasi ya kuiwakilisha nchi katika michuano ya CAF, ila nidhamu ndiyo kitu muhimu cha kuzingatia, hususan unapocheza na timu za madaraja ya chini.

“Unapocheza na timu za chini jambo la kwanza kwa wachezaji huchukulia ni mechi nyepesi na wanayoweza kufanya chochote, sasa hii ni hatari kwa sababu unapozidi kujiamini ndivyo ambavyo mpinzani wako pia anakushangaza,” alisema Josiah.

Kwa upande wa Kocha Mkuu wa African Sports, Khalid Adam alisema mechi dhidi ya Dodoma Jiji itakuwa ngumu kutokana na ubora wa wapinzani wao, ingawa hawatacheza kwa kuwahofia, isipokuwa watajilinda vizuri na kushambulia kwa kuwashtukiza.

RATIBA LEO IJUMAA

TRA United vs Kijiwe Nongwa (Saa 10:00 Jioni)

Dodoma Jiji vs African Sports (Saa 10:00 Jioni)

JKT Tanzania vs Hausang (Saa 10:00 Jioni)

KESHO JUMAMOSI

Pamba Jiji vs Transit Camp (Saa 10:00 Jioni)

Mashujaa vs Kengold (Saa 10:00 Jioni)

Geita Gold vs Nyika (Saa 10:00 Jioni)

Simba SC vs B19 (Saa 1:15 Usiku)

Namungo vs Kagera Sugar (Saa 10:00 Jioni)

MACHI 8, 2026

Mbeya City vs Bandari Tanzania (Saa 10:00 Jioni)

Fountain Gate vs Gunners (Saa 10:00 Jioni)

Mtibwa Sugar vs Mbuni (Saa 10:00 Jioni)

Tanzania Prisons vs TMA Stars (Saa 10:00 Jioni)

Azam FC vs Mbeya Kwanza (Saa 3:15 Usiku)

Singida BS vs Songea United (Saa 10:00 Jioni)

Coastal Union vs Stand United (Saa 10:00 Jioni)

Yanga vs Polisi Tanzania (Saa 1:15 Usiku)

YANGA YATAKATA SINGIDA, OKELLO AFUNGUA MLANGO

0

BINGWA mtetezi wa Ligi Kuu Bara, Yanga imeendeleza rekodi bora ya kutopoteza, baada ya kikosi hicho kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Singida Black Stars, katika mechi kali iliyopigwa leo Machi 5, 2026 kwenye Uwanja wa Airtel, mjini Singida.

Katika mechi hiyo, Prince Dube alifungua ukurasa wa mabao dakika ya 39, baada ya kupokea pasi nzuri ya Maxi Nzengeli, huku kiungo mshambuliaji, Mganda, Allan Okello akifunga la pili kwa mkwaju wa penalti dakika ya 45.

Okello aliyejiunga na kikosi hicho katika dirisha dogo la Januari 2026, akitokea Vipers ya kwao Uganda, alifunga bao hilo baada ya Dube kufanyiwa madhambi akiwa eneo la hatari na Mnigeria, Morice Chukwu.

Hata hivyo, licha ya Singida kucheza soka la kuvutia na kutengeneza mashambulizi ya mara kwa mara, lakini Yanga ilipata bao la tatu kupitia kwa kiungo, Mudathir Yahya dakika ya 54, akiunganisha mpira uliotemwa na kipa wa Singida, Metacha Mnata.

Ushindi huo kwa Yanga umeifanya timu hiyo kufikisha mechi 32 za Ligi Kuu Bara bila ya kupoteza, tangu mara ya mwisho kwa kikosi hicho kilipochapwa mabao 3-1 dhidi ya TRA United, zamani Tabora United, pambano lililopigwa, Novemba 7, 2024.

Katika mechi hiyo iliyopigwa Novemba 7, 2024, kwenye Uwanja wa Azam Complex, jijini Dar es Salaam, ilikuwa ni ya mwisho kwa kikosi hicho kupoteza ambapo kwa sasa imefikisha 32, huku kati ya hizo ikishinda 29 na kutoa sare tatu.

Kwenye mechi hizo 32 ilizocheza Yanga bila ya kupoteza tangu Novemba 7, 2024, kikosi hicho kimeshinda 29 na kutoka sare tatu, huku ikifunga mabao 99, wakati eneo la kujilinda limeruhusu nyavu zake kutikiswa mara nane.

Kabla ya mechi hiyo, Singida na Yanga zilikutana kwa mara ya kwanza katika uzinduzi wa Uwanja wa Airtel, Machi 24, 2025, ikiwa ni pambano la kirafiki lililoisha sare ya bao 1-1, huku ikishuhudiwa likichezwa dakika 57, baada ya kunyesha mvua kubwa.

Pia, Yanga imeendeleza rekodi bora dhidi ya Singida, kwani kabla ya mechi hiyo, mara ya mwisho zilipokutana katika Ligi Kuu, ilichapwa mabao 2-1,

Februari 17, 2025, yaliyofungwa na Clement Mzize dakika ya 14 na Prince Dube dakika ya 43.

Katika mechi hiyo, aliyekuwa mshambuliaji wa Singida, Jonathan Sowah, anayeichezea Simba msimu huu, ndiye mchezaji wa mwisho wa kikosi hicho kuifunga Yanga bao kwenye kichapo hicho cha Februari 17, 2025, ikiwa ni msimu uliopita wa 2024-2025.

Ushindi huo kwa Yanga umeifanya kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu, baada ya kufikisha pointi 32, katika mechi 12 ilizocheza hadi sasa msimu huu ambazo ni sawa za kikosi cha Singida kinachoshika nafasi ya tisa na pointi zake 19.

MASHABIKI WALITUPA LA KUJIVUNIA KARIAKOO DABI

0

HAWAKUWEZA kuujaza pomoni Uwanja wa New Amaan Complex unaoingiza watu 15,000 lakini baada ya mchezo wa Dabi ya Kariakoo, Machi Mosi, mwaka huu, mashabiki wa Simba na Yanga wametupa stori nzuri ya kusimuliana hapa kijiweni.

Jambo ambalo limefurahisha wengi ni namna mashabiki walivyoshabikia kistaarabu dakika 90 za mechi ya Watani wa Jadi, Yanga na Simba pasipo rabsha za aina yoyote.

Tofauti na tulivyowazoea zikikutanaga timu hizo kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, mashabiki hukaa majukwaa tofauti na wa Yanga hukaa sehemu yao na wa Simba kwao na ukienda kwa mwenzako unaweza kufanyiwa vurugu, juzi Zenji haikuwa hivyo.

Tumeona mashabiki wa vigogo hivyo vya soka nchini wakijichanganya na kukaa pamoja majukwaani na hakukuwa na purukushani wala vurumai ambazo zingefanya baadhi ya watu wasiondoke wakiwa salama.

Kwenye kijiwe hapa hatufahamu hilo limechangiwa na eneo lenyewe ambalo mechi imechezwa au tu mashabiki wa soka letu wameanza kubadilika hivi sasa lakini kinachotokea ni ishara nzuri sana kwa soka letu siku za usoni.

Mashabiki wameonyesha kumbe wanaweza kuitekeleza kwa vitendo dhana ya utani wa jadi uliopo baina ya timu hizo mbili badala ya kuzigeuza Simba na Yanga kama chanzo cha uhasama.

Ustaarabu huu ni utamaduni fulani mzuri ambao ukiendelezwa, soka letu litapiga hatua sana kwa vile tutatumia muda mwingi kujadili mambo mengi ya maana badala ya kufokasi na kutatua migogoro ambayo haina kichwa wala miguu.

Kilichoonyeshwa Zanzibar kinapaswa kuwa na mwendelezo hasa ukizingatia mwakani, nchi yetu itakuwa na tukio kubwa la Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) tunazoziandaa kwa pamoja na Kenya na Uganda.

Tunahitaji umoja wa mashabiki hasa wa Simba na Yanga katika kuisapoti timu yetu ya Taifa ‘Taifa Stars’ na mashindano kijumla.

SASA PESA NI NJENJE UKICHEZA VASO PSYCHO MERIDIANBET

0

Soko la burudani mtandaoni limepata msukumo mpya kupitia Meridianbet baada ya kuwasili kwa Vaso Psycho kutoka Expanse. Huu ni mchezo uliobuniwa kwa ajili ya wachezaji wanaopenda changamoto na wanaothamini maamuzi ya kimkakati. Si suala la kubonyeza na kusubiri, bali ni safari ya kuonesha uthubutu wako katika kila hatua. Vaso Psycho unafungua ukurasa mpya wa ushindani wa kisasa ndani ya kasino mtandaoni.

Kila raundi ya mchezo huu inakuja na hali ya kipekee inayomfanya mchezaji awe makini na mwenye maamuzi ya haraka. Unapocheza, unahamasishwa kufikiri tofauti na kujaribu mbinu mpya kila wakati. Msisimko wake unaongezeka kadri mzunguko unavyoendelea, ukikupa sababu ya kutaka kujaribu tena. Ni uzoefu unaounganisha akili na hisia kwa pamoja.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Kinachoufanya Vaso Psycho kuwa gumzo ni vizidishi vikubwa vinavyoweza kufikia hadi 10,000x pamoja na raundi maalum za bonasi. Hii ni fursa adimu kwa wale wanaotamani kuona dau lao likigeuka kuwa ushindi mkubwa. Kila mzunguko ni nafasi ya kubadili matokeo na kuandika historia yako ya mafanikio. Kwa wajasiri, hapa ndipo jukwaa lao halisi lilipo.

Ubunifu wake unaonekana wazi kupitia michoro ya kisasa na sauti zenye kuamsha ari ya ushindani. Mchezo umeandaliwa kwa viwango vya juu ili kumpa mchezaji hali ya kipekee ya burudani. Ni mchanganyiko wa teknolojia na ubunifu unaoleta ladha mpya kabisa sokoni. Hapa, kila sekunde ina thamani.

Jiunge leo kupitia tovuti ya meridianbet.co.tz au application ya simu na uanze safari yako na Vaso Psycho. Huu ndio wakati wa kuthubutu na kuonesha uwezo wako huku ukitarajia kupata ushindi wa kiwango cha juu.

DAR ES SALAAM DERBY HAITAWEZEKANA BILA FEITOTO

0

KIUNGO wa Azam FC, Feisal Salum maarufu kama Fei Toto, anatarajiwa kurejea kikosini na kuanza kucheza katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwemo ule dhidi ya Dodoma Jiji FC pamoja na dabi ya jijini dhidi katianga.

Fei Toto anakosa michezo miwili ya Azam FC, ukiwemo wa leo dhidi ya Tanzania Prisons FC katika ligi pamoja na mchezo wa hatua ya 32 bora ya CRDB Federation Cup dhidi ya Mbeya Kwanza FC, kutokana na kutumikia adhabu ya kadi nyekundu aliyopata katika mchezo dhidi ya Pamba Jiji FC.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Azam FC, Heshim Ibwe, kiungo huyo atakosekana katika michezo hiyo miwili pekee kabla ya kurejea uwanjani baada ya kumaliza adhabu yake.

“Fei Toto anakosa mechi mbili, ya leo dhidi ya Tanzania Prisons na ule wa Mbeya Kwanza katika Kombe la Shirikisho la CRDB. Baada ya hapo atakuwa amemaliza adhabu yake na ataweza kucheza michezo inayofuata ikiwemo dhidi ya Dodoma Jiji na Yanga,” amesema Ibwe.

Ibwe ameongeza kuwa kiungo huyo anaendelea vizuri na mazoezi ya timu ili kujiweka katika kiwango bora cha utimamu wa mwili, akilenga kurejea kwa nguvu kwenye kikosi cha Azam FC katika michezo muhimu ijayo.

Kurejea kwa Fei Toto kunatarajiwa kuipa nguvu zaidi Azam FC hasa kuelekea michezo mikubwa ya ligi, ikiwemo dabi ya Dar es Salaam dhidi ya Yanga ambayo huwa na ushindani mkubwa kila msimu.

SOWAH KITANZINI, SAA 72 KUJITETEA SIMBA

0

UONGOZI wa Simba SC umemtaka mshambuliaji wake, Jonathan Sowah, kutoa majibu rasmi ndani ya saa 72 sawa na siku tatu kuhusiana na tuhuma mbalimbali za kinidhamu zinazomkabili ndani ya klabu hiyo.

Imeelezwa kuwa nyota huyo amefikishwa mbele ya Kamati ya Nidhamu ya klabu, huku akitakiwa kuwasilisha majibu yake ndani ya muda uliotolewa. Wakati huo huo, adhabu yake ya kusimamishwa na kutokuwa sehemu ya kikosi cha timu inaendelea hadi uchunguzi wa kina utakapokamilika.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya klabu, uongozi wa Simba unahitaji maelezo ya kina kutoka kwa mchezaji huyo kuhusu vitendo kadhaa vinavyodaiwa kukiuka taratibu na nidhamu ya timu. Hatua hiyo inaelezwa kuchukuliwa kwa lengo la kulinda misingi ya uwajibikaji, heshima na nidhamu ndani ya kikosi hicho.

Chanzo kutoka ndani ya klabu kimeeleza kuwa miongoni mwa mambo anayopaswa kuyafafanua Sowah ni madai ya kufika kuchelewa kwenye mikutano ya timu pamoja na vipindi vya mazoezi, hali inayodaiwa kujirudia mara kadhaa na kuzua maswali kutoka kwa benchi la ufundi na uongozi wa klabu.

Mbali na hilo, mshambuliaji huyo pia anatuhumiwa kukataa kushiriki mazoezi ya ziada maarufu kama top-up sessions ambayo huandaliwa na benchi la ufundi kwa lengo la kuboresha utimamu wa mwili na kiwango cha wachezaji.

Sowah pia anatakiwa kutoa maelezo kuhusu tukio la kusafiri kwenda Angola akiwa amevaa jezi ya SL Benfica badala ya mavazi rasmi ya klabu, jambo linalodaiwa kwenda kinyume na taratibu za utambulisho wa timu wakati wa safari za kikazi.

Aidha, klabu hiyo inahitaji ufafanuzi wake kuhusu madai ya kufanya makosa ya makusudi uwanjani yanayoweza kusababisha adhabu kali kama kadi nyekundu. Matukio hayo yanatajwa kujitokeza katika baadhi ya michezo, ikiwemo dhidi ya Azam FC pamoja na Espérance Sportive de Tunis.

Inaelezwa kuwa baada ya kupokea majibu ya mchezaji huyo ndani ya muda uliowekwa, uongozi wa Simba utafanya tathmini na kuchukua hatua stahiki kulingana na kanuni na taratibu za klabu.

Hivi karibuni, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba, Crescentius Magori, amesema  kuwa endapo mchezaji huyo atabainika kuwa na makosa, klabu haitasita kuchukua hatua kali za kinidhamu ikiwemo adhabu au kukatwa sehemu ya mshahara wake.

SIMBA WAFUNGUA VITA KOMBE CRDB, B19 KWENYE MTEGO

0

LICHA ya mpinzani wao wa hatua ya 32 ya Kombe la Shirikisho la CRDB, B19, kuwa timu ya daraja la chini, uongozi wa Simba SC umesisitiza kuwa utaingia uwanjani kwa nguvu ileile iliyotumika katika mchezo wa Kariakoo Derby ili kuhakikisha wanapata ushindi.

Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema kikosi hicho kwa sasa kina ari mpya na kinaendelea kujipanga vyema kuelekea mchezo huo wa Jumamosi dhidi ya B19, maarufu kama Mabeberu wa Jiji.

Katika mchezo huo, Simba watakuwa wenyeji kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni jijini Dar es Salaam, mechi itakayopigwa saa 1:00 usiku.

Ahmed amesema umoja, nguvu na ushirikiano uliodhihirishwa na mashabiki, viongozi pamoja na wachezaji katika mchezo uliopita wa Kariakoo Derby, ni silaha muhimu ambayo wanahitaji kuibeba kuelekea pambano hilo.

“Umoja, nguvu na ushirikiano ambao mashabiki, viongozi na wachezaji wetu walionyesha katika mechi iliyopita ndio silaha tunayopaswa kwenda nayo siku ya Jumamosi dhidi ya B19,” amesema Ahmed.

Ameongeza kuwa baada ya mchezo wa Kariakoo Derby uliochezwa visiwani Zanzibar, timu imejifunza mambo mengi chanya na kuyafanyia kazi, hali iliyochangia kufanya kikosi hicho kuonekana kuwa na sura mpya uwanjani.

“Simba mpya imezaliwa pale Zanzibar. Tunachotakiwa sasa ni kuendelea kuwekeza nguvu kubwa katika michezo yetu ijayo ikiwemo huu wa Kombe la Shirikisho la CRDB dhidi ya B19 ili kuhakikisha tunasonga mbele kwenye mashindano hayo,” amesema.

Amesisitiza kuwa malengo ya Simba msimu huu ni kutwaa taji la kombe hilo, hivyo wanalazimika kujiandaa kwa umakini mkubwa ili kupata ushindi.

“Hata kama B19 ni timu ya daraja la chini, hatupaswi kuibeza. Tunaiheshimu lakini tunaingia uwanjani kwa lengo la kushinda na kusonga mbele,” ameongeza Ahmed.

Amesema Simba itaendelea kuwaheshimu wapinzani wake wote lakini hilo halitawafanya waingie uwanjani kwa tahadhari kupita kiasi, kwani dhamira yao ni kuendeleza kasi ya ushindi katika michuano hiyo.

329,001FansLike
12,344FollowersFollow
16,900SubscribersSubscribe

EDITOR PICKS