Uncategorized

AMUNIKE AENDELEZA DHARAU, ASISITIZA HANA CHA KULAUMIWA

admin July 2, 2019 10:20 am


Na Saleh Ally, Cairo
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Emmanuel Amunike ameendelea kusisitiza kwamba yeye hana cha kulaumiwa.

Amunike amesema mara baada ya Stars kupoteza mchezo wake wa mwisho katika michuano Afcon.

Taifa Stars ilifungwa mechi zote tatu za michuano hiyo kwa kukubali mabao nane katika mechi tatu huku ikifunga mawili.

Baada ya mechi ya mwisho baada ya Stars kulala kwa mabao 3-0 kutoka kwa Algeria, Amunike amuse a hana cha kulaumiwa.

“Nilaumiwe kwa lipi? Mimi ni kocha na timu uliiona. Hapo ndipo tulipofikia na nilichofanya sikuwa na zaidi ya kuongeza,” alisema.

Hata alipoulizwa kwamba ana maanisha hakuwa na uwezo wa kuongeza chochote cha kuiokoa au ana maanisha hakuwa na uwezo zaidi ya hapo, akajibu.

“Mimi nimemaliza, indigo tulipofikia, ahsante.”

MECHI ILIZOPOTEZA TAIFA STARS:
Vs Senegal 2-0
Vs Kenya 3-2
Vs Algeria 3-0

WAKATI UMEFIKA TUMEACHE AMUNIKE AENDE ZAKE SALAMA, TUSONGE SIMBA YAMALIZANA NA KIFAA KUTOKA TP MAZEMBE, KILIWAHI KUCHEZA KOMBE LA DUNIA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply