Home Uncategorized AZAM FC WABABE WA WACONGO KAZINI LEO FAINALI

AZAM FC WABABE WA WACONGO KAZINI LEO FAINALI


LEO kikosi cha Azam FC ambao ni wababe kwa timu zote za Congo walizokutana nazo ambazo ni TP Mazembe na Manyema FC kitakuwa na kazi ya kumenyana na KCCA ya Uganda kwenye mchezo wa fainali ya Kombe la Kagame uwanja wa Nyamirambo majira ya saa 12:00 jioni.

Azam FC ni watetezi wa kombe hili ambalo walilitwaa msimu uliopita kwa kuifunga Simba mabao 2-1 uwanja wa Taifa.

Walitinga hatua hii baada ya kuitungua mabao 2-1 TP Mazembe robo fainali na kushinda kwa penalti 5-4 dhidi ya Manyema FC hatua ya nusu fainali nchini Rwanda.

SOMA NA HII  SIMBA WAELEKEZA NGUVU ZAO LIGI KUU