Home Uncategorized YANGA: MSIMU UJAO TUTAFANYA MAAJABU

YANGA: MSIMU UJAO TUTAFANYA MAAJABU

MLINDA Mlango wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania, Metacha Mnata amesema kuwa msimu ujao lazima wapambane kufikia malengo ya timu kutokana na mipango waliyojiwekea.

Yanga imeweka kambi mkoani Morogoro kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao na hesabu zao kubwa ni kutwaa ubingwa uliopo mikononi mwa Simba.

“Kazi ipo msimu ujao ukizingatia kwamba kila timu imefanya usajili makini ni wakati wetu pia kuonyesha ushindani, imani yetu ni kubwa na tutafanya makubwa msimu ujao,” amesema.

SOMA NA HII  SARPONG: MUDA WANGU WA KUFUNGA BONGO UMEWADIA