Home Uncategorized HUYU NDIYE PILATO WA FAINALI YA AFCON KATI YA SENEGAL NA ALGERIA

HUYU NDIYE PILATO WA FAINALI YA AFCON KATI YA SENEGAL NA ALGERIA

BAMLAK Tessema mwenye umri wa miaka 39 raia wa Ethiopia ameteuliwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kuchezesha mchezo wa fainali ya michuano ya Afcon utakaochezwa Ijumaa kati ya Senegal na Algeria uwanja wa kimataifa wa Cairo.

Fainali inatajwa kuwa na msimko wa kipekee kutokana na timu zote mbili kuhitaji kuwa mabingwa wa michuano hii mikubwa.

Algeria na Senegal wote walikuwa kundi C ambapo walipokutana kwenye hatua ya makundi, Algeria waliibuka na ushindi wa bao 1-0.

SOMA NA HII  MORRISON ATAJA SABABU YA KUTUA NDANI YA YANGA