Home Uncategorized KAZI KUBWA YA MBELGIJI WA SIMBA IPO HAPA

KAZI KUBWA YA MBELGIJI WA SIMBA IPO HAPA

KOCHA wa Simba, Patrick Aussems amesema kuwa kwa sasa kikosi chake kina kazi kubwa ya kufanya kutimiza malengo yake kitaifa na kimataifa.

Simba kwa sasa ipo kambini nchini Afrika Kusini na imecheza mchezo mmoja wa kirafiki kwa ajili ya kusuka kikosi kipya dhidi ya Orbet Vet na imeshinda kwa mabao 4-0.

“Ni kazi kubwa na ngumu kuandaa kikosi hasa ukizingatia kwamba kazi yetu ni kusuka kikosi kipya ambacho kitakuwa na muunganiko mzuri.

“Kuna kazi kubwa ambayo tunapaswa kuifanya na kwa kuanza tunaunga muunganiko utakaosaidia kuwa na kikosi imara,” amesema.

SOMA NA HII  MWAMBA HUYU HAPA KUTOKA CHIPOLOPOLO AIUNGA MKONO POWER DYNAMO DHIDI YA SIMBA