Home Uncategorized KOCHA SIMBA AIBUKA NA LAKE BAADA YA KASEJA KUITWA STARS

KOCHA SIMBA AIBUKA NA LAKE BAADA YA KASEJA KUITWA STARS


Mchezaji wa zamani wa Simba Abdallah King Kibadeni, amesema kitendo cha Kocha Etienne Ndairagije kumuita Kipa Juma Kaseja kunako kikosi cha Taifa Stars ni maamuzi mazuri.

Kibadeni ameeleza kuwa kuitwa kwa Kaseja kutatoa nafasi kwa magolikipa wanaochipukia kujifunza mambo mengi kutoka kwake.

Kibadeni amesema bado Kaseja ana mchango mkubwa wakuendelea kuwepo kwenye kikosi cha Stars kutokana na uzoefu aliokuwa nao, akisema bado ana uwezo licha ya swala la umri kumtupa mkono.

Kaseja alijumuishwa kwenye kikosi kilichotajwa na Kaimu Kocha huyo mapema wiki hii ikiwa ni kwa mara ya kwanza Tangu mwaka 2013

SOMA NA HII  KOCHA WYDAD AWAANGALIA MASHABIKI WAO KISHA AKAWAPA HABARI HII.... HIKI NDICHO ITAKACHOAMBULIA SIMBA HUKO MARRAKESH