Home Uncategorized NDANDA, KAGERA SUGAR ZAIKOMALIA MWADUI FC

NDANDA, KAGERA SUGAR ZAIKOMALIA MWADUI FC

KLABU za Mwadui FC, Kagera Sugar na Ndanda FC zipo vitani kwa ajili ya kupata saini ya kiungo Abdallah Seseme.

Kiungo huyo bado timu yake ya Mwadui inahitaji huduma yake hali inayofanya kuwe na mvutano mkubwa kuipata saini ya nyota huyo.

Kocha wa Kagera Sugar, Mecky Maxime amesema kuwa mpango mkubwa wa kikosi chake ni kuboresha kikosi na kukifanya kiwe cha ushindani.

“Hesabu kubwa kwa sasa ndani ya Kagera Sugar ni kusuka kikosi bora na chenye ushindani, mipango ikikamilika kila kitu kitakuwa wazi,” amesema.

SOMA NA HII  JPM: MAKONDA UMESEMA UKIENDA MISRI TUTASHINDA? HAYA NENDA – VIDEO