Home Uncategorized NOMA!! HUU NDIYO UBALAA WA MIPANGO YA YANGA MSIMU UJAO – VIDEO

NOMA!! HUU NDIYO UBALAA WA MIPANGO YA YANGA MSIMU UJAO – VIDEO


Klabu ya Yanga imeadhimia kucheza mechi za kirafiki zisizo pungua Tano ili kujiimarisha kuelekea msimu ujao wa ligi kuu.

Akizungumza hii Leo na Waandishi wa habari jijini Dar es salaam Ofisa habari wa klabu hiyo, Dismas Ten,  amesema watacheza mechi hizo wakiwa morogoro pamoja na Dodoma ili kukiimarisha kikosi chake.

Hata hivyo Dismasi amesema Siku ya Wananchi ambayo walikuwa wamepanga imeahirishwa kutokana na michezo ya Timu ya taifa Huku wakisema watatangaza siku maalumu ya kufanyika mchezo huo.

Klabu ya Yanga ipo jijini Morogoro kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu Tanzania bara ambao unatarajiwa kuanza Agosti 28 mwaka huu.

SOMA NA HII  KAZI TATU ZA MOTO KWA YANGA KANDA YA ZIWA HIZI HAPA