BEKI wa kikosi cha Simba Gadiel Michael amesema kuwa kikosi cha Simba kipo imara tangu msimu uliopita jambo lililoipa ubingwa.
Gadiel kwa sasa yupo na Simba Afrika Kusini baada ya kusaini kandarasi ya miaka miwili akitokea Yanga.
“Simba ni timu bora na imara tangu msimu uliopita ndio maana iliweza kutwaa ubingwa, nina imani msimu ujao tutashirikiana vema kufanya vizuri na kufikia malengo,” amesema.
Simba ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara baada ya kutwaa mara mbili mfululizo kuanzia msimu wa 2017-18, 2018-19.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.