Home Uncategorized RAIS WA SHIRIKISHO LA MISRI AMPIGA CHINI KOCHA MKUU KISHA NAYE ABWAGA...

RAIS WA SHIRIKISHO LA MISRI AMPIGA CHINI KOCHA MKUU KISHA NAYE ABWAGA MANYANGA


BAADA ya timu ya Taifa ya Misri kutolewa hatua ya 16 bora na timu ya Afrika Kusini kwa kufungwa bao 1-0 jana uwanja wa Taifa wa Cairoimeripotiwa kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Misri, Hany Abourida amemtimua kocha Mkuu Javier Aguirre.

Bao la ushindi kwa Afrika Kusini lilifungwa na nyota Thembinkosi Lorch lilidumu mpaka mwisho wa mchezo huo uliokuwa na ushindani. 

Aguirre alikuwa na kandarasi ya miaka minne ndani ya kikosi cha Mapharaoh hao na alikuwa analipwa dola 120,000 kwa mwezi, pia imeripotiwa kwamba baada ya kutoa adhabu hiyo Rais huyo amejiuzulu nafasi yake pamoja na makamu wake naye Ahmed Shobeir naye amejiuzulu.

SOMA NA HII  JURGEN KLOPP AIPA TANO WATFORD KWA KUMTIBULIA REKODI YAKE MAZIMA