BAADA ya timu ya Taifa ya Misri kutolewa hatua ya 16 bora na timu ya Afrika Kusini kwa kufungwa bao 1-0 jana uwanja wa Taifa wa Cairoimeripotiwa kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Misri, Hany Abourida amemtimua kocha Mkuu Javier Aguirre.
Bao la ushindi kwa Afrika Kusini lilifungwa na nyota Thembinkosi Lorch lilidumu mpaka mwisho wa mchezo huo uliokuwa na ushindani.
Aguirre alikuwa na kandarasi ya miaka minne ndani ya kikosi cha Mapharaoh hao na alikuwa analipwa dola 120,000 kwa mwezi, pia imeripotiwa kwamba baada ya kutoa adhabu hiyo Rais huyo amejiuzulu nafasi yake pamoja na makamu wake naye Ahmed Shobeir naye amejiuzulu.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.