Home Uncategorized MBWANA SAMATTA AKOSA CHA KUWAAMBIA MASHABIKI

MBWANA SAMATTA AKOSA CHA KUWAAMBIA MASHABIKI

MBWANA Samatta, nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania anayekipiga klabu ya Aston Villa amesema kuwa hana cha kuwaambia mashabiki wa Tanzania zaidi ya asante kwa sapoti wanayompa.

Samatta alianza kazi rasmi ndani ya Aston Villa ambayo ilimpa kandarasi ya miaka minne na nusu akitokea Klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji. Mchezo wake wa kwanza ulikuwa ni wa nusu Fainali ya Kombe la Carabao dhidi ya Leicester City na ilishinda mabao 2-1.

Ndani ya dakika 65 alizocheza, Dean Smith, Kocha Mkuu wa Aston Villa alisema kuwa alifanya vizuri na anapaswa kupambana.

Samatta amesema:”Ni kazi ngumu kutafuta maneno ya kuwaambia mashabiki zangu wa Tanzania kwa sapoti ambayo wanaitoa, neno zuri ninaloliona ni kusema asante kwa sapoti, haina kufeli,”.

Kesho Samatta atakuwa na kibarua mbele ya Bounemouth ambao utakuwa ni wa kwanza kwake ndani ya Ligi Kuu England.

SOMA NA HII  NYOTA HAWA TISA NDANI YA SIMBA MSIMU UKIMEGUKA TU WANAWEZA KUSEPA BURE KABISA