Home Uncategorized KIVULI CHA YANGA CHAKWEPA NA TANZANIA PRISONS, SASA KUHAMIA DODOMA

KIVULI CHA YANGA CHAKWEPA NA TANZANIA PRISONS, SASA KUHAMIA DODOMA


TIMU ya Tanzania Prisons ya Mbeya imeamua kukimbia kivuli cha Yanga kilichokuwa inaitesa timu hiyo kwa kushindwa kupata matokeo chanya Uwanja wa Samora waliokuwa wanautimia kwenye mechi zake za karibuni.
Prisons iliyo chini ya Adolf Rishard baada ya kuchapwa na Yanga kenye mchezo wao wa 13 Uwanja wa Samora hawakupata ushindi zaidi ya kuambulia sare kwenye mechi mbili alizocheza hapo akiwa mwenyeji.
Kutokana  na maboresho yanayofanywa uwanja wa Sokoine uliokuwa unatumiwa na Prisons iliwalazimu watafute sehemu ya kuchezea na kuchagua Samora ambapo walikuwa wakipata taabu kushinda kwenye mechi zao zote tatu walizocheza.
Walipoteza kwa kufungwa na Yanga bao 1-0 bao la ushindi Ndanda ya bila kufungana kabla ya kuchapwa mabao 3-2 mbele ya Namungo FC  na kuwafanya wafungwe jumla ya mabao manne na walifunga mabao mawili pekee.
Mchezo wao unaofuata dhidi ya  KMC, Februari Mosi ambao ni wa ligi utachezwa Uwanja wa Jamhuri, Dodoma  badala ya Samora, Rishard ameliambia SpotiXtra kuwa uwanja wa mwanzo umekuwa ukimuumiza muda mrefu.
SOMA NA HII  KIDUKU AMTWANGA KWA TKO MTHAILAND