Home Uncategorized WALICHOKIAHIDI MTIBWA KWA YANGA NI MAUMIVU

WALICHOKIAHIDI MTIBWA KWA YANGA NI MAUMIVU


THOBIAS Kifaru, Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar amesema kuwa mchezo wao wa ligi dhidi ya Yanga hawana presha nao kwa kuwa wamejipanga kuwachapa mapema ili kuzibeba pointi tatu muhimu.

Mtibwa Sugar, jana, Januari,30 ilikuwa Uwanja wa Uhuru ikimenyana na Azam FC, itarejea tena uwanjani, Jumapili, kumenyana na Yanga iliyo chini ya Mbelgiji Lucy Eymael.

Kifaru alisema kuwa wana kazi ngumu ndani ya Bongo ila mawazo yao makubwa ni kushinda mbele ya Yanga mapema ili kupunguza kelele za mjini.

“Unajua timu yetu inatoka kijijini sasa ikishinda kwa hizi timu za mjini inapendeza sana na kuzima zile kelele, tumejipanga na tunatambua kwamba mapema tutashinda na kusepa na pointi tatu.

“Yanga wanaitambua vema Mtibwa, ninaamini wanatambua kwamba watacheza na Mabingwa wa Kombe la Mapinduzi, tuliwafunga Visiwani Zanzibar na kuwarejesha mjini mapema watataka kulipa kisasi kwa hilo wasahau, tunazijua mbinu zao tutawapa tabu,” alisema Kifaru.
SOMA NA HII  MASTAA WATAKAO IUA AL AHLY WAWEKWA WAZI SIMBA