Home Uncategorized BAADA YA KUBANWA MBAVU SASA AZAM FC KUGEUKIA UPANDE HUU

BAADA YA KUBANWA MBAVU SASA AZAM FC KUGEUKIA UPANDE HUU

BAADA ya kubwanwa mbavu na Mbeya City kwa kufungana bao 1-1 Uongozi wa Azam FC umesema kuwa sio mbaya kwa kuwa ilikuwa ni mechi ya ugenini.

Azam FC ilikubali sare ya kufngana bao 1-1 mbele ya Mbeya City kwenye mchezo uliochezwa jana, Februari,2 Uwanja wa Samaora, Iringa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Azam FC Jaffary Maganga amesema kuwa wachezaji walipambana ila bahati haikuwa yao.

“Wachezaji wamepambana kutafuta matokeo na bahati haikuwa yao mwisho wa siku tumeambulia pointi moja ugenini sio mbaya kwetu tunarejea kujipanga upya.

“Jumatano tutakuwa kazini mbele ya Prisons imani yetu ni kuona kwamba tunapata matokeo kwani tutakuwa nyumbani Uwanja wa Taifa,” amesema.

Azam FC ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 37 huku Mbeya City ikiwa nafasi ya 18 na pointi 14.

SOMA NA HII  MTIBWA SUGAR:: VIWANJA NI TATIZO,VIBORESHWE