Home Uncategorized HAJI MANARA WA SIMBA ALA DILI AZAM MEDIA

HAJI MANARA WA SIMBA ALA DILI AZAM MEDIA


HAJI Manara, Ofisa Habari wa Simba amepata dili la kuwa balozi wa bidhaa za Azam Media na Influencer (Mtu wa ushawishi kwenye mitandao) wa La Liga Experience 2020.

Mkataba huo amesaini leo Februari,3,2020 kwa ajili ya kufanya kazi na kampuni ya Azam Media.

Manara amesema kuwa ni mkataba mwingine utakaompa fursa adhimu ya kufanya kazi na kampuni kubwa zaidi ya habari lakini pia anaamini utaiwezesha kampuni kuendelea kutangaza bidhaa zake sambamba na ligi kuu ya Spain La Liga ambayo Azam tv wanaionyesha.


SOMA NA HII  MORRISON: NINGEPANDA NDEGE INGEKUWA DHARAU KWA WENZANGU...