Home Uncategorized ISHU YA YANGA KUTWAA UBINGWA MBELE YA SIMBA IPO NAMNA HII

ISHU YA YANGA KUTWAA UBINGWA MBELE YA SIMBA IPO NAMNA HII



Hivi ndivyo Saleh Jembe anavyoichambua Yanga na mikakati yake ya kutwaa ubingwa:-

Yanga bado haina mwendo mzuri maana iko katika nafasi ya nne baada ya kucheza mechi 22.

Ina viporo viwili mkononi, ikishinda vyote itafikisha pointi 46 na kukwea hadi nafasi ya pili lakini itakuwa tofauti ya pointi 16 na vinara wa ligi hiyo Simba.

Kumbuka mechi zilizobaki kama idadi itakuwa ni 14 ili ligi kumalizika.

Pointi 14 ni sawa na kushinda mechi karibu tano. Maana yake, si kazi nyepesi kwa Yanga kuwa bingwa. Pamoja na hivyo inaonekana kuna kazi ya ziada kwa Yanga kwenda vizuri na lazima kurekebisha mambo kadhaa na namna moja katika ufungaji.

Yanga imefunga mabao 25 huku Simba ikiwa imefunga 50, mara mbili yake. Azam FC imefunga mabao 31.

SOMA NA HII  KOCHA SIMBA AIPA TAHADHARI YANGA KWA ZESCO