Home Uncategorized KAGERA SUGAR YATUMA UJUMBE HUU KWA KMC

KAGERA SUGAR YATUMA UJUMBE HUU KWA KMC


KAGERA Sugar iliyo chini ya Kocha Mkuu, Mecky Maxime kesho itawakaribisha KMC kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho utakaochezwa Uwanja wa Kaitaba.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa majira ya saa 10:00 jioni, Februari 26.

Maxime amesema kuwa wanatambua aina ya kikosi wanachokutana nacho ni bora watatumia vema uwanja wa nyumbani kupata matokeo.

“Tutakuwa nyumbani na mashabiki watakuwa wetu hilo linatupa nguvu ya kwanza ya kupambana ukiachana na hilo maandalizi yapo vizuri imani yangu tutaoa burudani na kazi tutafanya.

“Mashabiki wajitokeze kwa wingi kuona namna tutakavyotoa burudani kwani kazi ni kazi kwetu uwezo tunao,”.

SOMA NA HII  SIMBA KUANZAKUTAMBULISHA MAJEMBE HAYA YA KAZI