Mechi namba 197- Singida United FC 2 vs Mwadui FC 2. Mchezaji wa Mwadui Hashim Yahya Mussa amepelekwa Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF).
Mchezaji amepelekwa kamatini kwa kosa la kuwaonyeshea kidole cha kati watazamaji kama ishara ya matusi baada ya filimbi ya kumaliza mchezo ilipopigwa.kitendo hicho kilifanyika katika mchezo uliofanyika February 8, 2020 katika uwanja wa Namfua mjini Singida.