Home Uncategorized MAMBO NI MAGUMU SASA NDANI YA SIMBA, MBELIGIJI ATOA LA MOYONI

MAMBO NI MAGUMU SASA NDANI YA SIMBA, MBELIGIJI ATOA LA MOYONI


MAMBO ni magumu ndani ya Simba kwa sasa baada ya kichapo cha bao 1-0 balaa zito limeibuka kwa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara kwa kusema kuwa majeruhi wengi ndani ya kikosi wanawaumiza.

Sven Vandernbroeck amesema kuwa ameshindwa kupata matokeo mazuri kutokana na kuwa na majeruhi wengi ndani ya kikosi jambo ambalo hana ujanja nalo.

“kiukweli nina majeruhi wengi ndani ya timu yangu wapo sita wote ni wa kikosi cha kwanza, matokeo ya kufungwa ni mabaya siwezi kusema moja kwa moja kwamba wamechangia la ni suala linalohitaji muda,” amesema.

Simba ipo nafasai ya kwanza kwenye msimamo ikiwa na pointi 50 baada ya kucheza mechi 20 za ligi.

Jana, Februari, 7 ilifungwa bao 1-0 na JKT Tanzania mchezo wa Ligi Kuu Bara wa kwanza kwenye mzunguko wa pili.

SOMA NA HII  KAKOLANYA ACHEKELEA MAISHA NDANI YA SIMBA