MBARAKA Yusuph, mshambuliaji wa Azam FC amerejea uwanjani baada ya kukaa nje kwa muda wa mwaka mmoja.
Mbaraka alikuwa anasumbuliwa na majeraha ya goti aliyoyapata wakati akiitumikia timu ya Namungo ambayo imepanda Daraja kwa sasa inashiriki Ligi Kuu Bara.
Habari kutoka Uongozi wa Azam FC zinaeleza kuwa Mbaraka alianza mazoezi rasmi jana, Februari 9, Jumapili na wachezaji wenzake wa Azam FC.
Yusuph alifanyiwa upasuaji wa goti lake la mguu wa kulia Aprili mwaka jana katika Hospitali ya Vincent Pallotti jijini Cape Town, Afrika Kusini, kufuatia kubainika kuchanika mtulinga wa kati wa goti hilo (Anterior Cruciate Ligament Tear).
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.