KOCHA wa Yanga, Luc Eymael anakibarua kizito cha kumenyana na Coastal Union, Februari 23 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Uwanja wa Mkwakwani.
Eymael amekiongoza kikosi chake kupata sare tatu mfululizo, ilianza mbele ya Mbeya City kwa kufungana bao 1-1 kisha ikifauata Tanzania Prisons ya bila kufungana zote Uwanja wa Taifa na ikalazimisha sare ya kufungana bao 1-1 mbele ya Polisi Tanzania Uwanja wa Ushirika, Moshi.
Atakutana na Coastal Union iliyo chini ya Juma Mgunda ambayo imetoka kupapaswa mabao 2-1 na Ruvu Shooting.
Mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Uhuru, Coastal Union iliacha pointi tatu Dar kwa kufungwa bao 1-0.
Charles Mkwasa, Kocha Msaidizi wa Yanga amesema kuwa wanawaheshimu wapinzani wao watapambana kupata matokeo mazuri.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.