Home Uncategorized YANGA:TUMEANDAA SARE KWA AJILI YA SIMBA

YANGA:TUMEANDAA SARE KWA AJILI YA SIMBA


UONGOZI wa Yanga umesema kuwa umejipanga kuona unapata matokeo chanya mbele ya Simba kwenye mchezo utakaochezwa Uwanja wa Taifa, Machi 8.

Mchezo wa kwanza ambapo Simba ilikuwa mwenyeji timu zote zilitoshana nguvu kwa kufungana mabao 2-2.

Antonio Nugaz, Ofisa Uhamasishaji wa Yanga amesema kuwa wamejipanga kuona namna gani watapata matokeo chanya kwenye mchezo huo.

“Kila kitu kipo sawa kwani sare zimeandaliwa kwa ajili ya mchezo huo na kazi itakuwa moja tu kutafuta matokeo chanya na hilo linawezekana mashabiki watupe sapoti,” amesema.

SOMA NA HII  LIVERPOOL YABAMIZA MTU MKONO