Beki wa Highlands Park ya Afrika Kusini, Abdi Banda amesimamishwa mazoezi kwa hofu huenda anaweza kuwa na ugonjwa wa Corona.
Taarifa za kutoka Afrika Kusini zimeeleza kuwa Banda amelazimika kwenda kuchukuliwa vipimo baada ya kugundulika amekuwa anakohoa na ana mafua makali.
“Wamesema pia ana mafua, hivyo amechukuliwa vipimo lakini kwanza ametakiwa kusimama mazoezi,” kilieleza chanzo.
Juhudi za kumpata Banda bado zinaendelea kufanyika lakini taarifa za kuchukuliwa vipimo tayari zimepatikana.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.