Home Uncategorized MANCHESTER CITY YABEBA UBINGWA WA CARABAO MBELE YA SAMATTA

MANCHESTER CITY YABEBA UBINGWA WA CARABAO MBELE YA SAMATTA


ASTON Villa timu anayokipiga Mbwana Samatta, jana Machi Mosi imeshuhudia ubingwa ukisepa jumla mpaka mikononi mwa wapinzani wao Manchester City.

Villa iliyo chini ya Dean Smith ilikubali kichapo cha mabao 2-1 kwenye mchezo wa fainali ya Kombe la Carabao iliyochezwa Uwanja wa Wembley.

City ilianza kuandika bao la kwanza dakika ya 20 kupitia kwa Arguero na bao la pili dakika ya 30 kupitia kwa Rodri.

Samatta alipachika bao dakika ya 41 kwa kichwa kilichozama nyavuni jumlajumla.

Timu ya mwisho kucheza na City fainali ilikuwa ni Watford na ilichapwa mabao 6-0 na alipocheza na Arsenal 2015 aliichapa 4-0 hivyo Samatta amefanya maajabu maana wengi walidhani ingechapwa mabao saba.

SOMA NA HII  ISHU YA KIUNGO MIQUISSONE NI NZITO KWA SIMBA, YAPIGA HODI FIFA