Home Uncategorized SIMBA KUIFUATA KMC KWA TAHADHARI HII LEO

SIMBA KUIFUATA KMC KWA TAHADHARI HII LEO


SVEN Vandnbroeck, Kocha Mkuu wa Simba amesema ataingia kwa tahadhari kubwa kuivaa KMC kutokana na ushindani uliopo ndani ya Ligi Kuu Bara.

Simba itaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kushinda mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Uhuru kwa mabao 2-0. 

Sven amesema: ‘Kwetu sisi kila mchezo ni muhimu kuona tunapata matokeo, ninawaheshimu wapinzani wangu na nitawafuata kwa tahadhari kubwa haina maana kwamba ukiwa bora haufungwi.

“Mashabiki wanapenda burudani na kuona timu inapata matokeo ni wakati wao kujitokeza kwa wingi kuona namna wachezaji wanavyojituma uwanjani,”.

Safu ya ushambuliaji ya Simba nayoongozwa na Meddie Kagre imefunga jumla ya mabao 50 ikiwa na pointi 62 kibindoni na ipo nafasi ya kwanza

SOMA NA HII  IBRAHIM AJIBU KWA SIMBA NDO BASI TENA MSIMU WA 2019/20