Home Uncategorized HIMID MAO:NILIPATA MUDA WA KUNUNUA MSOSI

HIMID MAO:NILIPATA MUDA WA KUNUNUA MSOSI


KIUNGO mtanzania Himid Mao anayekipiga Klabu ya ENPPI ya Misri amesema kuwa alipata muda wa kununua chakula kabla ya kuzuiwa kutoka ndani.

Nchini Misri, wakazi wa huko walizuiwa kutotoka nje tangu Machi 12 baada ya maambukizi kuanza ikiwa ni mpango wa Serikali kuzuia maambukizi zaidi.
Akizungumza na Saleh Jembe, Himid amesema kuwawalipewa muda maalumu wa kufanya manunuzi ya vyakula ambapo alinunua vya kutosha na kuweka akiba ndani.
“Nilipata muda wa kununa chakula ambacho niliweka ndani hivyo kwa muda huu ambao tunashinda ndani kuna hazina ya msosi, ila tunachokosa ni ule uhuru wa mwanzo kufanya mazoezi pamoja na wenzetu,” amesema Himid.
SOMA NA HII  MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI JUMATANO