Home Uncategorized HUMUD ACHEKELEA DILI LA KUJIUMGA NA YANGA, AZUNGUMIZA MAISHA YAKE NDANI YA...

HUMUD ACHEKELEA DILI LA KUJIUMGA NA YANGA, AZUNGUMIZA MAISHA YAKE NDANI YA MTIBWA SUGAR

ABDULHAMAN Humud nyota anayekipiga ndani ya Mtibwa Sugar amesema kuwa maisha anayoishi ndani ya kikosi hicho anayapenda na yanampa furaha kwa sasa.

Humud amekuwa akihusishwa kujiunga na Yanga msimu ujao jambo ambalo mwenyewe amekuwa akisema likikamilika itakuwa ni furaha nyingine kwake.

Akizungumza na Saleh Jembe, Humud amesema :”Maisha yangu kwa sasa yapo ndani ya Mtibwa Sugar na ninaishi kwa amani na furaha pia ikiwa itatokea nikaondoka nitaweka wazi kwani ukiwa mchezaji lazima kila kitu kiwe wazi,”

Kabla ya Ligi Kuu Bara kusimamishwa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona, kiungo huyo alikuwa ametupia mabao mawili kati ya 22 yaliyofungwa na Mtibwa Sugar.

SOMA NA HII  MECHI ZA AWALI NDANI YA LIGI KUU BARA KUANZIA SEPTEMBA 6