Home Uncategorized KAGERA SUGAR WAWAOMBA MASHABIKI KUENDELEA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA

KAGERA SUGAR WAWAOMBA MASHABIKI KUENDELEA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA


MECKY Maxime, Kocha Mkuu wa Kagera Sugar amesema kuwa ni muhimu kwa wachezaji na mashabiki kuendelea kuchukua tahadhari juu ya Virusi vya Corona.

Akizungumza na Saleh Jembe, Maxime amesema kuwa kila mmoja ni wajibu wake kuchukua tahadhari na kujilinda dhidi ya Virusi vya Corona. 

“Kila mmoja ni wajibu wake kuchukua tahadhari na kujilinda dhidi ya Virusi vya Corona kwani wakati uliopo kwa sasa wa maabukizi ni muhimu kila mmoja kujilinda.

“Wachezaji pia na mashabiki ni muhimu kutambua kwamba afya ni bora na ili iwe bora inabidi ilindwe,” amesema.

SOMA NA HII  FAMILIA YA MARADONA YAANZA KUVURUGANA KISA MALI