Home Uncategorized MTUPIAJI POLISI TANZANIA AWAOMBA WATANZANIA KUENDELEA KUCHUKUA TAHADHARI

MTUPIAJI POLISI TANZANIA AWAOMBA WATANZANIA KUENDELEA KUCHUKUA TAHADHARI


SIXTUS Sabilo, nyota wa Polisi Tanzania amesema kuwa kwa sasa anaendelea kuchukua tahadhari ya kujilinda dhidi ya Virusi vya Corona akiwa zake Bunda.

Nyota huyo mwenye mabao saba ndani ya Ligi Kuu Bara huku akitupia mabao mawili kwa penalti ni miongoni mwa wazawa wenye ngekewa ya kutupia mabao.

“Jambo la msingi ni kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona kwani hili janga lipo hivyo ni muhimu kuchukua tahadhari ili kuwa salama.

“Natumia muda mwingi nikiwa na familia nyumbani jambo hili linanifanya niwe makini muda mwingi kujilinda mimi na jamii yangu kiujumla,” amesema.

SOMA NA HII  MHILU ATUMA UJUMBE HUU WA KWA MEDDIE KAGERE