Home Uncategorized MWAMBA WA LUSAKA CHAMA ATAJA MASHARTI YA KUTUA YANGA

MWAMBA WA LUSAKA CHAMA ATAJA MASHARTI YA KUTUA YANGA

CLATOUS Chama, nyota anayekipiga ndani ya Klabu ya Simba amesema kuwa Yanga haiwezi kuipata saini yake msimu ujao wa mwaka 2020/21 kutokana na kuwa mali ya Simba labda msimu unaofuata wa mwaka 2021/22.

Chama amekuwa kwenye sarakasi za usajili msimu huu ambapo Yanga ilielezwa kuwa inaitaka saini yake jambo lililowafanya Simba kupelekea malalamiko Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kile walichoeleza kuwa Yanga wamekiuka utaratibu wa usajili.

Akizungumzia ishu ya kutua Yanga Chama amesema:”Kuhusu kuhitajika na Yanga ni jambo zuri ila kwa msimu ujao haitawezekana labda ule unaofuata inawezekana.

“Lakini yote yatakuwa sawa ikiwa utaratibu wa usajili utafuata na makubaliano yakawa sawa,” amesema.

Mkataba wa Chama unameguka mwaka 2021 aliongeza mkataba wa miaka miwili msimu wa 2018/19.

SOMA NA HII  KILICHOIPOTEZA YANGA UWANJA WA UHURU MBELE YA KMC HIKI HAPA