METACHA Mnata, mlinda mlango namba mbili wa Yanga amesema kuwa sababu kubwa iliyomfanya ajiunge ndani ya Yanga ni ushindani wa namba uliokuwa ndani ya kikosi cha Azam FC.
Mnata alisajiliwa na Yanga ambapo alikuwa anakipiga Mbao FC kwa mkopo akitokea Azam FC ambao ndio walikuwa mabosi zake.
“Nilijiunga na Yanga baada ya Azam FC kukubali kwa kuwa wao walikuwa wananimiliki na walikuwa wamenipeleka Mbao FC ili kujiweka sawa.
“Ushindani ndani ya Azam FC ulikuwa mkubwa na haikuwa rahisi kupata nafasi ndani ya kikosi cha kwanza jambo lililosababisha pia nikaibukia Mbao FC,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.