Home Uncategorized YANGA YAWATAKA MASHABIKI KUCHUKUA TAHADHARI YA CORONA

YANGA YAWATAKA MASHABIKI KUCHUKUA TAHADHARI YA CORONA

UONGOZI wa Ya

nga umesema kuwa mashabiki wanapaswa waendelee kuipa sapoti timu yao na kuendelea kujikinga na Virusi vya Corona.


Ligi Kuu Bara imesimama kwa muda kutokana na kusambaa kwa Virusi vya Corona ambavyo vinatikisa dunia kwa sasa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Mhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz amesema kuwa kwa sasa ni muhimu kwa mashabiki kuendelea kuchuka tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona na kuendelea kuipa sapoti timu yao.

“Kila mmoja anatambua kwamba tupo kwenye kipindi kigumu cha mpito ila nina amini kwamba kila wakati ni bora kuendelea kupeana sapoti na kuchukua tahadhari ya Virusi vya Corona.

“Ni kipindi kigumu kwani kuna vingi ambavyo tunavikosa ila hamna namna lazima maisha yaendelee.” amesema.
SOMA NA HII  LIGI KUU BARA KWA SASA IMEMEGUKA MAKUNDI MANNE