Home Uncategorized AJIBU KUTOKUWEPO NDANI YA SIMBA MSIMU UJAO

AJIBU KUTOKUWEPO NDANI YA SIMBA MSIMU UJAO

INAELEZWA kuwa msimu huu wa 2019/20 utakuwa wa mwisho kwa kiungo mshambuliaji wa Simba Ibrahim Ajibu kukipiga ndani ya Simba.

Ajibu alitua Simba akitokea Yanga

kwa kusaini dili la miaka miwili kwa Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Bara.

Taarifa zinaeleza kuwa baada ya TP Mazembe kumkatia tamaa ya kumpata kuna timu nyingine nje ya nchi ambayo inahitaji kupata saini yake.

“Ajibu hatakuwepo tena msimu ujao ndani ya Simba iwapo dili lake la kucheza nje ya nchi litakamilika, jina la timu inayomhitaji limefichwa kwa kuhofia mpango kuvurugika,” ilieleza taarifa hiyo.

Patrick Rweyemamu Menena Mkuu wa Simba amesema kuwa hajapata taarifa hizo.

SOMA NA HII  NYOTA WAPYA SIMBA WAANZA MATIZI, MORRISON KAMA KAWAIDA HAISHIWI JAMBO