Home Uncategorized MCHEZAJI HUYU SIMBA ALIKUWA ANAMPASUA KICHWA SVEN

MCHEZAJI HUYU SIMBA ALIKUWA ANAMPASUA KICHWA SVEN

SVEN Vandenbroec, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa miongoni mwa vitu ambavyo vilikuwa vinampasua kichwa ni kukosa huduma ya Miraj Athuman,’ Sheva’.

 Sheva alikuwa kwenye ubora wake ndani ya Simba ilikuwa kwenye mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar fainali ya Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar ambapo alitonesha majeraha ya fundo la goti mbele ya Mtibwa Sugar.

Sven amesema:-“Miongoni mwa vitu ambavyo nilikuwa ninaumia ni kukosa huduma ya Miraj kutokana na kutokuwepo uwanjani kwake, alikuwa ni mchezaji muhimu lakini majeruhi yalimfanya awe nje kwa muda. 


“Ninaamini atarejea kwenye ubora wake kutokana na kupata matibabu kwa wakati ambapo alikuwa nje ya uwanja.”

 Sheva ametupia mabao sita na ametoa pasi moja ya bao lililofungwa na Meddie Kagere.

SOMA NA HII  TANZANIA PRISONS V SIMBA KINAWAKA KESHO SOKOINE